24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Ole Nasha apokea mabomba ya maji Ngorongoro

Na Janeth Mushi, Arusha

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, William Olenasha amepokea mabomba na vifaa vyenye thamani ya Sh milioni 246.

Mabomba hayo na vifaa hivyo vinatarajiwa kutekeleza miradi ya maji katika vijiji vya Piyaya, Kisangiro, Masusu, Sale, Olaika, Samunge, Digodigo na Sanjani, wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha.

Katika hafla hiyo fupi iliyofanyika katika Ofisi za RUWASA, Ngorongoro Julai 26, 2021, Olenasha ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo hilo aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Raymond Mwangwala, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ngorongoro, Ndirango  Laizer na Mwenyekiti wa Halmashauri, Emanuel Shangai.

Wengine ni, Mwenyekiti wa UWT Wilaya, Fatma Ngorisa na Wajumbe wengine wa Kamati ya Siasa ya CCM wilaya ya Ngorongoro.

Olenasha amesema kuwa Tangu kuanzishwa kwa RUWASA wilaya ya Ngorongoro ameona kuwa miradi ya maji ikitekelezeka na amesisititiza miradi yote ya maji itekelezwe kwa wakati ili wananchi wapate huduma ya maji.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles