23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

MONGELLA AVUNJA KIKAO CHA WADAU WA ELIMU

Na JUDITH NYANGE,

MKUU wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella  jana alilazimika kuvunja kikao cha wadau wa elimu wa mkoa  baada ya wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, maofisa elimu wa msingi na sekondari  kutoka baadhi ya halmashauri kutohudhuria.

Kikao hicho cha wadau wa elimu Mkoa wa Mwanza kilipangwa kufanyika kuanzia saa 2:00 asubuhi   kujadili hali halisi ya elimu.

Mambo mengine ni changamoto zinazoikabili sekta hiyo  na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto  zilizopo na barua za mwaliko wa kikao hicho zilitolewa miezi miwili iliyopita.

Lakini hadi    saa 3:18 asubuhi  wakurugenzi wote wa halmashauri za wilaya za mkoa huo walikuwa  hawajawasili katika ukumbi wa mikutano.

 Mongella ambaye alikuwa ndiye mwenyekiti wa kikao hicho  alisema ana taarifa ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga, aliyekwenda kushughulikia mgogoro wa ardhi na si wengine.

Hata hivyo aligundua kutoalikwa  kwa wadau muhimu katika kikao hicho kikiwamo Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Mwanza,  Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSA) mkoa.

Alisema wakurugenzi wengi hawakuwapo wakati   maofisa elimu ya msingi na sekondari walituma wawakilishi katika kikao hicho.

Mpaka saa 3:20 asubuhi viongozi wa wilaya waliokuwapo   ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Dk. Leornard Masale,  Mkuu wa Wilaya ya Magu, Hadija Nyembo,    Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba, Pendo Malabeja, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosa,  Crispin Luanda   na baadhi ya maofisa elimu msingi na sekondari.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles