24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

MBUNGE ALIA TATIZO LA UPATIKANAJI MAJI DAR

RAMADHAN HASSAN,

MBUNGE wa Viti Maalumu, Salma Mwasa (CUF), amehoji ni lini Serikali itatekeleza miradi ya maji  Dar es Salaam.

Akiuliza swali la nyongeza   bungeni jana, Mwasa alidai  miradi mingi ya maji   Dar es Salaam imekuwa haitekelezwi, je ni lini Serikali itaanza kuitekeleza.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Nyamagana, Stanslaus Mabula (CCM),  alihoji ni lini Serikali itahakikisha kuwa wananchi wa Nyamagana wanapata maji ya uhakika hasa ikizingatiwa  wamezungukwa na Ziwa Victoria.

‘’Jimbo la Nyamagana lina ukubwa wa kilomita za miraba 256, kati ya hizo kilomita za mraba 71.56 ni eneo la maji ya Ziwa Victoria.

“Lakini bado wananchi wake hawapati maji ya uhakika ya bomba, sasa ni lini Serikali itahakikisha wananchi hao wanapata maji?” alihoji Mabula,

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Isaack Kamwelwe alisema Serikali imekwisha kukamilisha miradi ya maji katika Mto Ruvu chini na juu.

Alisema kufanya  hivyo huduma ya maji itakuwa ya uhakika   Dar es Salaam.

Kamwelwe alisema huduma ya maji katika Wilaya ya Nyamagana  Mwanza inatolewa kwa asilimia 90 ya wakazi wote  na wilaya hiyo.

‘’Hata hivyo baadhi ya wakazi ambao wanaishi katika sehemu za mwinuko   na wanaoishi  pembezoni mwa Jiji wanakosa ya maji,’’ alisema.

Alisema kwa kutambua hilo imepata mkopo wa masharti nafuu kutoka European Investment Bank (EIB)   Euro milioni 54 (Sh bilioni 110).

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles