27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, May 2, 2024

Contact us: [email protected]

Binti wa Papa Wemba amtoa machozi Rais Kabila

*Asema amekufa kwa mapenzi ya Mungu

*Baba wa Koffi aliyekuwa nguli wa soka naye afariki

NA NOAH YONGOLO

“KIFOO kifoo, kifoooo kifoo, kifoo hakina huruma…, ndivyo wanavyokumbuka wakazi wa Kongo na wapenda muziki kwa ujumla duniani kote katika kuomboleza vifo vya watu wawili mashuhuri katika muziki wao.

Baba wa Koffie Olomide aliyefarikiBaba wa mwanamuziki nguli barani Afrika, Koffi Olomide ‘Mopao Mokonzi’ anayetamba na wimbo wa ‘Selfie’, Charles Agbeba aliyekuwa mcheza mpira maarufu nchini humo katika timu ya AS Vita ya nchini Kongo.

Mzee huyo amefariki dunia Jumamosi iliyopita akiwa nchini Ufaransa huku Koffi akitoa shukrani kwa wasanii mashuhuri waliofika nyumbani kwake na kumfariji kutokana na kumpoteza baba yake huyo.

Leo nguli wa muziki Papa Wemba anatarajiwa kupumzishwa katika nyumba yake ya milele nchini humo, baada ya kufariki akiwa jukwaani akifanya shoo nchini Ivory Coast.

Rais Kabila atoa machozi

Rais wa Kongo (DRC), Joseph Kabila, alijikuta akishindwa kujizuia hadi machozi yakamtoka aliposikia salamu maalumu za familia kutoka kwa binti wa kwanza wa Papa Wemba, Tellier Shungu Anaendo Caddy.

Binti huyo alianza salamu hizo kwa kusema kwamba ni wajibu wao kutoa salamu za heshima na shukurani kwa Rais wao Kabila kwa msaada mkubwa alioutoa kufanikisha mazishi ya baba yao mpendwa.

Binti huyo alizungumzia baadhi ya kumbumkumbu ambazo wengi hawazifahamu akisema kuwa baba yake amefariki kwa mapenzi ya Mungu, ingawa wanakabiliwa na kazi ngumu ya kumzungumzia baba yao aliyekuwa kipenzi na rafiki wa watu hasa raia wa Kongo DR.

Congolese singer Papa Wemba performs durAliendelea kusema kuwa baba yao alikuwa akiitunza na kuilea kwa upendo na ukarimu uliopindukia familia yao. Hakusita kuwachukua watoto yatima na kuishi nao kama familia moja, Caddy aliendelea kusema wanajivunia kuwa na baba aliyekuwa na tabia nzuri kwa kuwafundisha mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuwa na tabia nzuri, utu na maadili mema.

Binti huyo alimuelezea baba yake kuwa na uwezo mkubwa wa kuchanganya maisha ya kiasili na ya kisasa, huku akikumbuka kwamba baba yao amekufa akiaacha ahadi kwa mjukuu wake, Ambre ambaye ni mtoto Caddy kwamba angekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha harusi yake.

Ripoti ya daktari

Caddy anasema kabla ya marehemu baba yake, Papa Wemba hajakwenda nchini Ivory Coast kuhudhuria tamasha aliloalikwa, daktari wake alimthibitishia kwamba alikuwa na afya nzuri ndiyo maana walimruhusu kwenda huko.

“Msiba kwa familia za Kiafrika ni alama tosha ya umoja, ushirikiano, kusameheana na kuimarisha uhusiano hivyo raia wote wa Kongo DR katika kipindi hiki cha maombolezo tuwe wamoja, kifo cha mzee Wemba kiwe chanzo cha kuamsha ari ya uzalendo na utamaduni wa Kongo na nyanja za kimataifa.

“Kifo cha baba yangu kiwe jukwaani, kiwe chanzo cha kuunganisha historia ya tamaduni za nchi mbili, Kongo DR na Ivory Coast,’’ alimaliza binti huyo na kuwatoa machozi watu wengi waliokuwa wakimsikiliza kwa makini.

Nyimbo zatungwa

Katika hatua nyingine wanamuziki mbalimbalia akiwemo, Adolphe Dominguez wa bendi ya Wenge Tontatonya, ametunga wimbo maalumu kwa ajili ya marehemu Papa Wemba ‘Embleme De La Musique Africaine (Nembo ya muziki wa Kiafrika).

Katika wimbo huo aliouimba kwa hisia kali za kuomboleza, amemuelezea Wemba kuwa ni mfalme wa muziki wa rhumba na askari wa muziki wa Kongo DR pia amezitaja baadhi ya nchi mbalimbali za Afrika pamoja na Asia, Ulaya kwamba nao wanamlilia.

Ratiba ya mazishi

Katika ratiba ya mazishi iliyotolewa na Serikali ya nchi hiyo chini ya kamati ya maandalizi iliyowashirikisha baadhi ya ndugu wa marehemu, wanamuziki, waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali na Wizara ya Mawasiliano na Utamaduni, inasimamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Jiji la Kinshasa, Andre Kimbuta.

Ratiba hiyo ilianza juzi katika viwanja vya Bunge la nchi hiyo mwili wa marehemu Wemba uliagwa huku Rais Joseph Kabila akimtunuku nishani maalumu kisha mwili wake ukarejeshwa nyumbani kwake katika Kijiji cha Molokai.

Kisha mwili wa nguli huyo ulirudishwa tena kwenye viwanja vya Bunge ambapo wageni mbalimbali walialikwa kutoa salamu zao za mwisho wakishirikiana na wananchi wa kawaida na kusogezwa mbele hadi leo ili watu wengi waweze kuuaga mwili huo.

Wakati hayo yakiendelea shuhuda mbalimbali za kumuelezea nguli huyo, kuweka mashada ya maua na bendi yake aliyoiacha ilikuwa ikipiga nyimbo za kuomboleza, huku vikundi mbalimbali vya ngoma na muziki navyo vikipata nafasi ya kuomboleza msiba huo mkubwa.

Kwa heri Papa Wemba

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles