29.2 C
Dar es Salaam
Monday, September 16, 2024

Contact us: [email protected]

‘Beauty Queen’ Yazidi Kumpaisha Director P

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Staa wa muziki mwenye asili ya Afrika anayeishi nchini Canada, Director P, ameendelea kujizolea umaarufu kupitia wimbo wake mpya, Beauty Queen. Wimbo huo umeonekana kuvutia mashabiki wengi, hasa kwenye mtandao wa YouTube, na kumfanya Director P kuzidi kung’aa katika ulimwengu wa muziki.

Director P, ambaye ni rapa na mwongozaji wa video za muziki, amewashukuru mashabiki wake kwa mapokezi makubwa ya Beauty Queen.

“Afrika ni nyumbani, na ninapata sapoti kubwa sana kutoka kwa mashabiki wa pande hizo. Ngoma yangu ya Beauty Queen imewagusa wengi wanaopenda rapa kutokana na jinsi nilivyoonyesha ufundi wa kumsifia mwanamke ninayempenda,” alisema Director P.

Ameongeza kuwa anashukuru familia yake, hasa mke wake kipenzi, kwa sapoti kubwa wanayompa kwenye sanaa yake, jambo ambalo linampa nguvu ya kuendelea kufanya makubwa kwenye tasnia ya muziki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles