25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

‘ASILIMIA 80 YA BIASHARA NCHINI SI RASMI’

                                                                 |Derick Milton, Bariadi



Mwenyekiti wa Bodi ya Mpango wa kuratibu na kurasimisha Biashara Tanzania (Mkurabita),  Balozi Ole Njoolay amesema asilimia 80 ya biashara nchini na asilimia 89 ya ardhi siyo rasmi.

Njoolay amesema hayo leo Alhamisi Julai 26, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, mkoani Simiyu.

Amesema ili nchi iweze kuwa na uchumi mzuri lazima angalau ifikie kiwango cha asilimia 25 ya kurasimisha biashara zake.

“Ili Tanzania iweze kukua kiuchumi lazima wafanyabishara wawe wanarasimisha biashara sanjari na ujenzi wa vituo vya urasimishaji nchini,” amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles