30.2 C
Dar es Salaam
Friday, May 3, 2024

Contact us: [email protected]

AJALI ZA BODABODA ZINACHANGIA ONGEZEKO LA WENYE MATATIZO YA UBONGO

Ajali za pikipiki maarufu bodaboda, zimechangia matatizo ya ubongo kiwango kikubwa kulinganisha na ajali nyingine.

Mbali na ajali za bodaboda, kuanguka kwenye mti nayo inadaiwa kuongeza idadi ya Watanzania wenye matatizo ya ubongo hasa kupasuka kwa mishipa ya fahamu na saratani ya ubongo.

Daktari Bingwa wa Upasuaji Ubongo na Mishipa ya Fahamu wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), Samuel Swai amesema leo kutokana na hali hiyo serikali hulazimika kuwapatia rufaa ya matibabu wagonjwa kati ya saba hadi nane kwenda nchini India ambako yanatolewa katika utaalamu wa kiwango cha hali ya juu.

“Ingawa Moi ina uwezo wa kufanya upasuaji wa ubongo hata hivyo hulazimika kuwapatia rufaa wagonjwa ambao huhitaji huduma ya kibingwa zaidi kwenda India kwa sababu bado hatujitoshelezi Kwa upande wa vifaa na gharama za matibabu ni kubwa ambapo mgonjwa mmoja hugharimu kati ya Sh milioni 20 hadi 25 kufanikisha upasuaji ambazo serikali hugharamia,” amesema.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles