25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Mtaalamu wa chanjo aliyefutwa kazi asema Marekani itakabiliwa na hali mbaya zaidi ya corona majira ya baridi

 WASHINGTON, MAREKANI 

OFISA wa zamani wa ngazi ya juu wa afya nchini Marekani ameliambia bunge la congresi kuwa Marekani inaweza kukabiliwa na hali mbaya kuwahi kushuhudiwa wakati wa majira ya baridi kwa sababu ya virusi vya corona.

Rick Bright aliongoza shirika la serikali kujaribu kutengeneza chanjo, lakini akaondolewa katika kazi hiyo mwezi uliopita.

Awali alisema aliondolewa kazini kwa kuelezea hofu juu ya tiba zinazotangazwa na rais Donald Trump.

Rais Trump alimfuta kazi kwa madai kuwa alikua mtumishi asiyeridhika.

Bright pia aliiambia kamati ya Bunge la wawakilishi ya masuala ya afya kuwa maisha yanapotea kwa sababu ya serikali kutochukua hatua katika hatua za mwanzo za mlipuko wa virusi vya corona.

Alisema kuwa kwa mara ya kwanza alizungumzia juu ya ukosefu wa zana za matibabu mwezi Januari, na kufikisha suala hilo katika ngazi za juu za Wizara ya Afya na huduma za binadamu (HHS), lakini hakujibiwa.

Wakati wa ushahidi, Bright alionya kwamba dirisha la kushughulikia virusi vya corona linakaribia kufunga.

“Kama tutashindwa kuboresha jinsi tunavyokabiliana na ugonjwa huu sasa, kwa misingi ya sayansi, ninaogopa janga litakua baya sana na kuendelea kwa muda mrefu,” alisema.

“Bila mpango bora, 2020 unaweza kuwa na kipindi kibaya zaidi cha majira ya baridi kuwahi kushuhudiwa katika histioria ya sasa”.

Bright pia ameiambia kamati hiyo ya bunge la wawakilishi kuwa mwezi Januari alipokea barua pepe ambayo hawezi kusahau, kutoka kwa wasambazaji wa barakoa za hospitali ambao walioonya juu ya upungufu mkubwa wa vifaa hivyo.

“Alisema… tunahitaji kuchukua hatua.Na nikaituma barua hiyo kwa ngazi ya juu ya HHS – na sikupata jibu.

Alisema a kuondolewa kwake kazini kulikua ni matokeo ya kuendelea kwake kusisitiza kwamba fedha zilizotengwa na congress za kupambana na mlipuko wa virusi zinapaswa kuwekwa katika suluhu salama na zilizochunguzwa kisayansi na sio katika dawa, chanjo au teknolojia nyingine ambazo hazijathibitishwa kisayansi.

“Nilizungumza wazi wakati ule, na ninatoa ushahidi leo, kwa sababu sayansi sio siasa au upendeleo -lazima iongoze katika njia ya kupambana na virusi,” aliongeza.

Malalamiko yaliyowasilishwa mapema mwezi huu, yanasema Bright aliondolewa kwenye wadhfa wake kama Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti wa kimatibabu – Biomedical Advanced Research and Development Authority (Barda) kwa sababu za kisiasa.Bright anasema aliondolewa muda mfupi baada ya taarifa kuhusu chloroquine, ambayo alisema alikuwa chanzo chake.

Rais Trump alikua amesema kuwa hydroxychloroquine, dawa ya malaria ina uwezekano wa “kuleta mabadiliko “ katika tiba ya Covid-19-ingawa wataalmu wengi wamesema kuwa huenda isiwe ya ufanisi, au hata ikawa hatari.

Malalamiko ya Bright yalikua ni kwamba aliamua kuzungumza na waandishi wa habari kwa sababu maofisa wa serikali walikataa kusikia tahadhari zake. Alisema alikua na jukumu la kujaribu na kulinda umma kutoka kwa madawa ambayo anaamini ni ya hatari kwa usalama na afya ya umma.

MAJIBU YA TRUMP 

Baada ya kusikia, Rais Trump aliwaambia waandishi wa habari : “Simfahamu.Sijawahi kukutana nae.Sitaki kukutana nae.”

“Lakini nilimtazama , na anaonekana kama mtu mwenye hasira, mtumishi asiyeaminika , ambaye kusema kweli kwa mujibu wa baadhi ya watu hakufanya kazi nzuri sana .”

Waziri wa afya, Alex Azar alidai kuwa maofisa walifuata mapendekezo ya Bright.

“Kila alichokilalamikia kilifanikiwa-anachokizungumzia kilifanyaka ,” alisema Azar

“Alisema alizungumzia kuhusu haja ya kupata vifaa vya kusaidia kuongeza oksijeni kwenye mapafu.Tuliagiza vifaa hivyo(respirators) kutokana na maagizpo ya rais.

Alisema tunahitaji mradi wa Manhattan wa chanjo. Tukawa na Mradi wa Manhattan.”

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles