24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Makonda azindua soko la madini na vito

Brighiter Masaki

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, leo jumatano Julai 17, amezindua soko la kimataifa la madini na vito jijini Dar es salaam, ikiwa ni utekelezaji wa agizo alilotoa Rais Dk. John Magufuli kwa kutaka kila mkoa kuwa na soko hilo.

Akizungumza Makonda amesema uwepo wa soko hilo litasaidia wananchi kununua madini na vito halali na kupunguza matapeli waliokuwa wakiuzia wananchi na Wageni madini na vito feki.

Aidha Makonda amesema uzinduzi wa soko hilo umekuja wakati muafaka ambao Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa wakuu wa nchi za SADC ambao wataingia nchini mwezi ujao wakiambatana na wafanyabiashara amapo anaamini watapata nafasi ya kutembelea soko hilo

“Kama tunavyojuwa Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa wakuu wa nchi za SADC ambao wataingia nchini mwezi ujao wakiambatana na wafanyabiashara ambapo pia ninaamini watapata nafasi ya kutembelea soko hili” amesema Makonda.

Aidha amesema ndani ya soko hilo yanapatikana madini ya aina zote hivyo amewataka wananchi kulitumi soko hilo kwani ni halali na linatambulika na serikali.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles