29.3 C
Dar es Salaam
Thursday, May 2, 2024

Contact us: [email protected]

QUEEN DARLIN AFICHUA KINACHOIBEBA WCB

Na JESSCA NANGAWE


MWANADADA pekee kutoka kundi la WCB, Mwajuma Abdul ‘Queen Darling’, amesema kundi hilo limekuwa likifanya vizuri kutokana na umoja na nidhamu waliyojiwekea.

Akizungumza na MTANZANIA, Queen Darling ambaye ni dada wa kiongozi wa lebo hiyo ya Diamond Plutnumz, amesema wasanii wa kundi hilo kila mtu anaelewa dhumuni la kuwepo hapo na ndio maana hawajawahi kutetereka tangu kundi lianzishwe.

“Ni sheria ambazo wenyewe tunajiwekea hasa malengo yetu ya kuhakikisha tunatimiza kile tulichokusudia, kikubwa nidhamu tumeipa kipaumbele sana na ndio maana hujawahi kusikia Wasafi wana tatizo lolote na mtu,” alisema.

Alisema wamekuwa wakifanya ushindani wa kimaendeleo ambao umezidi kuwapa motisha ya kufanya kazi, huku kila mmoja akijiona ana deni kubwa ndani ya kundi hilo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles