25.2 C
Dar es Salaam
Sunday, April 28, 2024

Contact us: [email protected]

LUKUVI AVUNJA NYUMBA YAKE KUPISHA UJENZI WA BARABARA

Na FRANCIS GODWIN, IRINGA

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliam Lukuvi ambaye pia ni Mbunge wa Ismani, ameivunja nyumba yake iliyopo Mapogoro, Ismani kama njia ya  kumuunga mkono Rais John Magufuli  katika ujenzi wa barabara ya kiwango  cha  lami  kati ya  Iringa kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Akizungumza jana mara baada ya  kushiriki zoezi la ubomoaji wa nyumba   hiyo, Waziri Lukuvi, alisema kuwa akiwa kama kiongozi ameamua kuwa  wa kwanza kuonyesha mfano kwa  kuanza  kuivunja  nyumba hiyo ambayo  kimsingi sehemu  ya  robo ilikuwa imepigwa alama ya X nyekundu na  robo  tatu  ilipigwa alama ya X ya kijani, ila kutokana na kuunga mkono jitihada za  Serikali katika ujenzi wa barabara   hiyo,  ameamua kuivunja yote na hatadai  malipo yoyote.

“Kimsingi barabara hii ya kuelekea  Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ilianza  kabla ya sisi kuja kujenga hivyo barabara  tuliikuta hakuna hata mmoja kati yetu ambaye barabara  ilimkuta na haya  ni maendeleo yetu sote na Taifa kwa  ujumla, mimi nilijenga jirani na  barabara ili kuwapungia watu mikono  wakati wanapita sikujua kama ni  barabarani, ila  baada ya kujulishwa nimeamua kwa  mikono yangu kuja  kuvunja nyumba yangu.”

Waziri Lukuvi alisema Serikali haitalipa  fidia  yoyote  kwa  wananchi  waliojenga  nyumba  katika  hifadhi ya  barabara  akiwamo yeye mwenyewe, hivyo alitaka wananchi wote ambao walivunja sheria  kwa kutojua waanze kuvunja nyumba  zao  wenyewe kwa  hiari bila kusubiri  kuvunjiwa.

Alisema kuwa wananchi wote  waliowekewa alama ya X katika  nyumba zao, kuanza  kuvunja pasipo  kusubiri kujiuliza na maana ya alama  nyekundu ama kijani, kwani barabara   hiyo ilianza toka miaka 30 hivyo hifadhi  ya Ruaha na barabara hiyo ilianza kabla ya hapo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles