29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, May 1, 2024

Contact us: [email protected]

Happiness-Mwanamke aliyebamba fursa uuzaji  bidhaa za mkonge Kimataifa

Na Esther Mnyika, Mtanzania Digital

Mkonge ni moja kati ya  zao la biashara Tanzania,asili ya zao hili ni Mexico na baadae likasambaa katika nchi za India na Tanzania mwaka 1892.

Inaelezwa kuwa zao la Mkonge liliingizwa nchini na mtaalamu wa kijerumani Dr.Richard Hindorff ambaye alikua mtafiti wa mimea na udongo.

Kutokana na mabadiliko ya tabianchi yaliyopo sasa, zao hili linaweza kuwa mbadala kwa maeneo ya vijijini kwani zao la Mkonge lina sifa za kustahimili hata kwenye maeneo ambayo mazao mengine hayawezi kustawi.

Mwaka 2019 Serikali ilitangaza zao la mkonge kuwa moja kati ya mazao saba ya kimkakati hapa nchini.

Kutokana na hilo Serikali imeiagiza Bodi ya Mkonge Tanzania kwa kushirikiana na wadau wote kuhakikisha kuwa uzalishaji wa zao la mkonge unaongezeka kutoka tani 36,000 mwaka 2019 kufikia tani 120,000 ifikapo mwaka 2025.

Mkakati huo pia unahusisha maeneo mbalimbali ikiwamo kuhamasisha na kushirikisha wakulima wadogo na upatikanaji wa masoko.

Mahitaji makubwa ya mkonge kwa sasa ni kuzalisha bidhaa mpya kama vile composite kwa ajili ya viwanda vya magari na shughuli za ujenzi, Sukari, pombe kali, karatasi maalum.

Nchi ambazo ni wanunuzi wakuu  ni China, Saudi Arabia, Nigeria, India, Uhispania, Ujerumani, Moroko, Japani ,Kenya na Israel.

Happiness Nyitu ni mmoja wa Watanzania walioona fursa  katika zao la mkonge ambapo kwa sasa ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Sisal Fibre L.t.d inayohusika na uuzaji wa nyuzi za mkonge.

Mfanyabiashara huyo anasema  alianzisha kampuni  mwaka 2020, ambapo tayari inafanya viziri katika kuuza bidhaa za mkonge  ndani na nje ya nchi.

Anasema  kwa sasa soko lake lipo barani Asia,  Ulaya na Afrika, huki akitarajia kufungua  kampuni  nyingine Afrika Magharibi  mwanzoni wa mwaka 2024.

“Tuna kiwanda kidogo cha kuchakata mkonge  katika level za kuuza ndani na nje ya nchi tunanunua mkonge sehemu mbalimbali za mikoa nchini ikiwemo Manyara, Mara, Simiyu, Shinyanga,  Singida,  Morogoro,  Dodoma,  Tanga na mikoa mingine inayozalisha mkonge,”amesema Nyitu.

Amesema wamekuwa wakinunua kwa wakulima wadogo ambao wanakuwa wamechakata nyuzi kwa kiasi baada ya hapo wanapeleka kiwandani kuchakata kwa ngazi  za kimataifa .

“Kwa nini niliingia kwenye biashara  ya kuuza nyuzi zitokanazo na mkonge? Ni kutokana na historia tuliyonayo ilinifanya nijiulize kwa nini hatuuzi mkonge kama zamani nini kinasababisha?, “amesema.

Amesema alifanya utafiti mdogo na kugundua kwamba nyuzi za plastiki zimechukua sehemu kubwa za mkonge lakini bado zao hilo  lina matumizi mengi.

Nyiti anasema wanaendelea kufanya utafiti ili kuweza kutengeneza bidhaa nyingine za mkonge  kulingana na ukuaji wa teknolojia.

Anaeleza kiwa nyuzi wanazalisha  zinazotumika kutengeneza vifaa vya ujenzi,  mbolea, chakula cha mifugo na vitu vingine.

Amesema soko la ndani wanafanya kwa asilimia ndogo kwa sababu  wamewaachia wajasiriamali ambao bado mitaji yao ni midogo na hawezi kuuza soko la nje.

Amesema mkonge  ni kama dhahabu na kujivunia mafanikio aliyopata kupitia biashara hiyo ikiwamo kupanua soko lake.

“Mafanikio mengine  ni ongezeko la uchumi  kila anaye shiriki kwenye biashara ya mkonge na nimewapatia ajira vijana na wakina mama, haya ni mafanikio, “amesema.

Akizungumzia kuhusu changamoto zinazowakabili ni kushindwa  kufikia masoko  kwa urahisi  pia uchakataji kwani wanahitaji mashine bora ili kutoa mkonge wenye ubora wa juu.

Changamoto nyingine ni gharama za usafiri  zimepanda na upatikanaji  wa mikopo  ya kilimo kwa wanaojihusisha  na uchakataji wa mkonge na biashara.

Aidha Nyiti akizungumzia kongamano la wanawake katika biashara chini ya mkataba wa eneo huru la biashara Afrika(AfCFTA) lililofanyika kwa siku tatu na  kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali kutoka nchi 55 Afrika, jijini Dar es Salaam, anasema anajivunia kwani ameweza kupata cheti cha kumtambua.

Anaeleza kuwa Januari, 2023  alishiriki mkutano ulioandaliwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dk.Ashatu Kijaji  alieelezea soko huru eneo la biashara na kampuni ambazo zipo tayari  kusafirisha mkonge  kupitia makubaliano ya soko huru  la Afrika.

“Nilimuahidi kuwa nipo tayari  kll kusafirisha kupitia soko huru la Afrika, mnamo Agosti  mwaka huu nilipata cheti cha uhalisia wa bidhaa kupitia soko huru la Afrika (Certificate living Under AfCFTA)  na hiki cheti cha kwanza  kupitia mkutano  huu,”ameeleza.

Amesema yeye ni mwanamke  wa tatu  nchini  kusafiri bidhaa  kwenda soko huru la Afrika na mwanamke wa kwanza kusafirisha  mkonge  kupitia soko hilo na faida walizopata kuongeza wateja na kuendeleza kutangaza zao la mkonge.

Ameeleza  kufanyika kwa kongamano hilo  ni chachu ya kuhamasisha wanawake  wengine kufanya biashara  katika  soko hilo,fursa zipo nyingi hivyo wachangamkie.

Nyiti anasema matarajio ambayo wanategemea kupitia kongamano hilo ni masoko  mapya na wateja ndani ya bara na ongezeko  la matumizi  ya mkonge  katika ngazi zote na kupanda kwa uchumi Afrika.

“Itasaidia ‘social economic development’  kwa wanawake, mojawapo  kwenye kujishughilisha na kazi za mkonge shambani na viwandani  na biashara ipo wazi kikubwa kufuata utaratibu na sheria zilizowekwa, “amesema.

Ameongeza kuwa wanawake wanatakiwa kuwa wengi kufanya biashara katika soko hilo kwa sababu ni walengwa wa kwanza na kujiunga katika vikundi kuweza kufanya biashara.

Nyiti ameshauri  katika sehemu wanazofanya kazi kuwepo na vitendea kazi kati ya mama na mtoto itawasaidia  kuongeza uzalishaji wa bidhaa.

“Kama kinara  wa usafirishaji wa bidhaa kwenye soko huru la Afrika naamini  watakuja wanawake wengi zaidi na nipo tayari kuwaongoza njia wanawake wenzangu  katika soko hili wakati ndo sasa na milango ipo wazi,”amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles