BAADA ya kimya kirefu katika muziki wa kizazi kipya, Dayna Nyange ameibuka na kutangaza kurudi upya kwa ‘surprise’ ya wimbo mpya na mipango mipya katika mwaka huu.
Dayna alisema mwaka uliopita alishindwa kwenda na wakati, ndiyo maana hakufanya vizuri sana, lakini mwaka huu amejipanga kwenda na kasi ya muziki, huku akidai wimbo anaotaraji kuuachia ni ‘surprise’ kwa mashabiki wake.
“Mashabiki wangu wamekosa vitu vingi, ikiwemo shoo zangu za nguvu, nyimbo zangu za mahaba na makeke yangu niwapo jukwaani, lakini wasiwe na hofu, kwa kuwa nimerudi upya kuwatetea kiburudani,’’ alijinadi Dayna.