Katika akaunti yake ya Istagram, Lupita ameandika kwamba amekasirishwa na namna ambavyo watu weusi hawajajumlishwa katika tuzo hizo, badala yake kupewa nafasi ya kuwa wagawaji wa tuzo hizo kwa watu weupe.
“Ni jambo la kusikitisha sana kuona tuzo hizo mwaka huu zinawapa watu weupe wakati wapo weusi wanaofanya vizuri na wanastahili kutwaa, huu ni ubaguzi wa rangi na haina maana yoyote,” aliandika Lupita.
Mwaka 2014 Lupita alishinda tuzo hiyo kutokana na uwezo wake ambao aliuonesha katika filamu ya Twelve Years a Slave.