UJIO mpya wa bendi ya Double M Plus unatarajiwa kufanyika muda mfupi baada ya bendi hiyo kuwasili nchini ikitokea nchini Msumbiji.
Bendi hiyo itawasili mwishoni mwa wiki hii baada ya ziara ya kimuziki iliyofanya nchini humo na pia kuweka kambi ya mazoezi iliyochukua zaidi ya miezi miwili.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Muumini Mwinjuma ‘Kocha wa Dunia’, alisema baada ya kumaliza maonyesho yao katika miji mbalimbali nchini humo, bendi hiyo iliweka kambi ya mazoezi ambapo ilisukwa upya ili iwe tishio na shindani kwa bendi nyingine zilizopo nchini.
“Bendi imeiva, tupo kamili kutoa burudani na tunawataka mashabiki wetu wawe tayari kutupokea kwa nyimbo za karne tulizowaandalia sambamba na shoo za kutosha,” alieleza.