28.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 30, 2024

Contact us: [email protected]

19 MBARONI BIASHARA DAWA ZA KULEVYA IRINGA

Na FRANCIS GODWIN-IRINGA

VITA ya dawa za kulevya iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, imevuka mipaka na sasa imetua mkoani Iringa ambako watuhumiwa 19, wakiwamo wafanyabiashara na watumiaji wametiwa mbaroni.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza, alisema mapambano hayo sasa yatakuwa endelevu kama njia ya kukomesha biashara hiyo.

“Pamoja na kuwakamata watuhumiwa ambao wanahusishwa na biashara hii, si wao tu, pia tumewakamata hata watumiaji ili kuweza kupata maelezo ya kina ni wapi wanaponunua na nani anawauzia.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Julius Mjengi, alisema Jeshi la Polisi litaendelea na msako mkali ili kuweza kuwatia mbaroni watu wanaofanya biashara hiyo na watumiaji.

Alisema kuwa kati ya watuhumiwa hao, 14 ni ‘mateja’ ambao wameathirika kwa utumiaji wa dawa za kulevya na watano ni wafanyabiashara wa dawa hizo haramu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles