28.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 30, 2024

Contact us: [email protected]

Sekondari mpya tano kufunguliwa Musoma vijijini

Na Shomari Binda, Musoma

Jumla ya Sekondari mpya tano zinatarajiwa kufunguliwa katika Jimbo la Musoma vijijini mkoa wa Mara ili kupunguza wingi wa wanafunzi madarasani na kutembea umbali mrefu.

Kukamilika kwa madarasa hayo kunatokana na ushirikiano mkubwa uliopo baina ya nguvu za wananchi na mbunge wa jimbo hilo, Prof. Sospeter Muhongo.

Akizungumza na Mtanzania Digital Katibu wa mbunge huyo, Hamis Gamba amesema kukamilika kwa shule hizo kutafikisha jumla ya shule 27 za sekondari zikiwemo mbili za binafsi.

“Kata ya Lifulifu ni moja ya kata ambazo zilikuwa hazina shule ya sekondari na kwa sasa tunakamilisha shule hizo,” amesema Gamba.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles