29.2 C
Dar es Salaam
Saturday, May 18, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali: Tutaendelea kuunga mkono uzazi salama

*Ni baada ya UNFPA na UK AID kuikabidhi vifaa vya uzazi wa mpango

Na Faraja Masinde, Mtanzania Digital

Serikali imeeleza kuwa itaendelea kuunga mkono uzazi salama kwani unasaidia afya ya mama na kumwezesha mtoto kuwa na utimamu mzuri wa mwili na akili.

Hayo yameelezwa Septemba 26, 2023 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Mama na Mtoto, Wizara ya Afya, Dk. Ahmad Makuwani, katika hafla ya kupokea vifaa vya uzazi wa mpango vilivyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi(UNFPA) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uingereza nchini.

Dk. Makuwani amesema kuwa uzazi salama unasaidia siyo tu kwa mama bali hata upande wa mtoto unakuwa bora kwani ananyonyeshwa kikamilifu hatua inayochochea matokeo bora pindi anapokuwa darasani.

“Tunaposheherekea siku hii ya Uzazi Salama tukumbuke kwamba uzazi salama ni kitu cha muhimu kwani inahakikisha kwamba mwanamke anakuwa na nafasi kati ya mimba moja hadi nyingine hatua inayomwezesha kuwa na afya bora.

“Pia inamwezesha mtoto kuwa na lishe bora hasa kwa walio chini ya miaka mitano, hivyo inasaidia matokeo bora na uelewa mkubwa kwa mtoto pindi awapo darasani. Serikali tutaendelea tutaendelea kufanya kazi na wadau wetu wa maendeleo ikiwamo kuwapa ushirikiano pindi unapohitajika ili kuhakikisha kwamba huduma hizi za uzazi wa mpango ambazo zipo kwenye miongozo na sera zetu zinapatikana kwa kila mhitaji ili kufikia lengo la kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi.

“Kwani ukiangalia katika vipaumbelea vilivyozungumziwa uzazi wa mpango ni namba moja na Tanzania sasahivi takwimu zetu zote zinaonyesha kwamba tumeweza kupunguza vifo vya uzazi kwa asilimia 50, haya ni matokeo vifaa hivi vinavyotolewa nawashirika wetu wa maendeleo kwa kuongozwa na kinara UNFPA,” amesema Dk. Makuwani.

Akizungumzia vifaa hivyo, Mwakilishi Mkazi wa UNFPA, Mark Bryan Schreiner amesema kuwa vifaa hivyo walivyokabidhi kwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ambao ni Ubalozi wa Uingereza vina thamani ya Dola za Marekani milioni 9.5 (zadi ya Sh bilioni 21) ambapo dola milioni 7.5 ni kutoka UNFPA na dola milioni 1.9 ni kutoka Ubalozi wa Uingereza kupitia Maendeleo ya Kimataifa UK AID.

“Bidhaa hizi zilinunuliwa kuanzia Julai 2022 hadi sasa na kutoa njia za kisasa za uzazi wa mpango za kutosha kutosheleza mahitaji ya wanandoa milioni 3 kwa mwaka mmoja.

“Kutokana na ununuzi huu, tulizuia makadirio ya mimba zisizotarajiwa 1,473,532, vifo vya uzazi 1,958, na utoaji mimba usio salama 400,620 na kuokoa GBP 112,909,979 katika huduma ya afya ya moja kwa moja. Mafanikio haya yanawezekana tu kwa ushirikiano wetu wa kina na wa muda mrefu na Serikali ya Tanzania,” amesema Schreiner.

Sehemu ya vifaa hivyo.

Amesema uzazi wa mpango ni taarifa, njia na mbinu zinazoruhusu watu binafsi kuamua kama na lini wapate watoto. Hii ni pamoja na aina mbalimbali za vidhibiti mimba – ikiwa ni pamoja na tembe, vipandikizi, vifaa vya ndani ya uterasi, taratibu za upasuaji zinazozuia uwezo wa kuzaa, na njia za vizuizi kama vile kondomu – pamoja na mbinu zisizo vamizi kama vile njia ya kalenda na kujizuia.

“Kupanga kwa bidii pia kunajumuisha taarifa kuhusu jinsi ya kupata mimba wakati? inawezekana, pamoja na matibabu ya utasa. UNFPA inaunga mkono vipengele vingi vya upangaji uzazi wa mwezi, ikiwa ni pamoja na kununua vidhibiti mimba, kutoa mafunzo kwa ‘wataalamu wa afya kuwashauri watu binafsi kwa usahihi na kwa umakini kuhusu chaguzi zao za kujamiiana, na kukuza elimu ya kina ya kujamiiana shuleni,” amesema Schreiner.

Ameongeza kuwa, uzazi wa mpango ni taarifa, njia na mbinu zinazoruhusu watu binafsi kuamua kama ni lini wapate watoto.

‘Hii ni pamoja na aina mbalimbali za vidhibiti mimba – ikiwa ni pamoja na tembe, vipandikizi, vifaa vya ndani ya uterasi, taratibu za upasuaji zinazozuia uwezo wa kuzaa, na njia za vizuizi kama vile kondomu – pamoja na mbinu zisizo vamizi kama vile njia ya kalenda na kujizuia.

“Kupanga kwa bidii pia kunajumuisha taarifa kuhusu jinsi ya kupata mimba wakati? inawezekana, pamoja na matibabu ya utasa. UNFPA inaunga mkono vipengele vingi vya upangaji uzazi wa mwezi, ikiwa ni pamoja na kununua vidhibiti mimba, kutoa mafunzo kwa ‘wataalamu wa afya kuwashauri watu binafsi kwa usahihi na kwa umakini kuhusu chaguzi zao za kujamiiana, na kukuza elimu ya kina ya kujamiiana shuleni,” amesema Schreiner.

Mkurugenzi wa Maendeleo kutoka Ubalozi wa Uingereza, Kemi Williams.

Awali, Mkurugenzi wa Maendeleo kutoka Ubalozi wa Uingereza, Kemi Williams alisema: “Athari za upangaji uzazi ni zaidi ya afya. Ni za kisekta nyingi na hata za vizazi. Imethibitishwa vyema kuwa uboreshaji wa afya na lishe ya mtoto una uwezo wa kuathiri vyema utendaji na tabia za kitaaluma. Kwa upande mwingine, elimu ni kigezo muhimu cha uchukuaji uthabiti katika matumizi ya huduma za uzazi wa mpango,” alisema Kemi.

Warren Bright, Mkuu wa Mawasiliano kutoka UNFPA.
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles