31.2 C
Dar es Salaam
Saturday, May 18, 2024

Contact us: [email protected]

UWT yatoa msaada kwa wananchi wa Hanang

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania UWT, Mary Chatanda  akikabidhi Msaada  Mbalimbali kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Jenista Mhagama leo Desemba 5, walipowatembelea wakiwa wajumbe wa Kamati ya Maafa ya UWT na Viongozi wa Mikoa ya Manyara na Arusha katika kuwapa pole walioathirika na mafuriko hayo.

Chatanda amesema kwa hakika huu msiba mzito ambao umeshtua Taifa na kila mtu na wao kama Umoja wa wan awakeanawake Tanzania wamejikusanya kwa umoja wao kuleta Msaada huu ambao utasaidia kwa wananchi wa Hanang. 

“Sisi tulikuwa Rufiji kwenye Tamasha la Kumuenzi Bibititi Mohamed, lakini tukapata taaharifa hii na baadae tukaona kwenye  Vyombo mbalimbali vya Habari  tukasema kweli hali ni mbaya ndivyo  tukaketi na kamati yangu ya Utekelezaji tukaamua tuje na hiki  kidogo kwa ajili ya kurejesha tabasamu  kwa watu ambao wamepata shida hii,” amesema Chatanda. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles