23.1 C
Dar es Salaam
Sunday, September 8, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali yawaahidi wawekezaji kutatua changamoto zao saa 24

Na CLARA MATIMO- MWANZA, SIMIYU

SERIKALI  imesema ipo tayari  kupokea wawekezaji muda wowote  katika sekta mbalimbali  pamoja na kusikiliza changamoto zao ili  waweze kufanya biashara katika mazingira mazuri.

Hayo yalibainishwa jana na Mkurugenzi mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC), Dk. Maduhu Kazi,  baada ya kupokea shule ya sekondari  iliyojengwa katika  Kijiji cha Bugatu Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza  na chuo cha ufundi  kilichopo kijiji cha    Kasori wilayani Busega mkoa wa Simiyu vilivyojengwa na kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginnery vyenye  thamani ya Sh. milioni 330.

Alisema TIC muda wote milango ipo wazi ili kuhakikisha inakuwa na taarifa za kila mwekezakaji na kujua kama anakabiliwa na changamoto

yoyote na kuitatua kwa  haraka kwa kuwa Serikali inahitaji wawekezaji ambao wako tayari kuisaidia jamii kuinua uchumi.

“Katika kufanikisha hilo kwa sasa tunatumia  teknolojia ya kisasa kwenye mawasiliano na wawekezaji, tunatumia ofisi za kanda zilizopo jijini Mwanza ili kuhakikisha kila mfanyabiashara anawekeza katika mazingira yasiyokuwa na usubufu ama urasimu, watu wanaotaka kuwekeza waje TIC bado kuna fursa nyingi,”alisema na kuongeza;

“Kiwanda cha Alliance Ginnery kimezingatia maagizo ya serikali ya awamu ya tano, tunahitaji  wawekezaji kama hawa ambao wanaisaidia jamii inayowazunguka siyo wawekezaji wanaokwenda kuchimba mashimo mawili ya choo halafu wanasema wameisaidia jamii,”  alisema. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Magu ambako shule hiyo imejengwa, Salum  Kalli, alikishukuru kiwanda hicho kwa msaada  huo na kubainisha kwamba  kimesaidia kutatua changamoto ya watoto  kutembea umbali mrefu kwenda shule.

Naye Meneja wa kiwanda cha Alliance Ginnery, Boaz  Ogola, alisema wametoa msaada huo wa shule uliyogharimu Sh milioni 150  baada ya kuona watoto wa eneo hilo wanatembea umbali mrefu kwenda shule  pia wamejenga chuo cha ufundi kilichogharimu Sh milioni 180 baada ya kubaini  wanaomaliza elimu ya msingi wanakosa fursa ya kupata elimu ya ufundi ili iwasaidie kujiajiri.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka,  baada ya kukabidhiwa chuo cha ufundi aliagiza wasichana wote waliomaliza darasa la saba kuanza kusajiliwa ili waanze kupata mafunzo pia aliwasisitiza   wazazi  na walezi kuacha kupokea mahari  kuwaozesha  watoto wao wa kike waliomaliza darasa la saba.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles