25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Rudiger ataka mil. 640

BEKI wa Chelsea, Antonio Rudiger, amewashika pabaya mabosi wa klabu hiyo baada ya kuwaambia wampe Pauni 200,000 (zaidi ya Sh mil. 640 za Tanzania) kwa wiki kama wanataka asaini mkataba mpya.

Mkataba wake utafikia ukomo Juni, mwakani, na kwa sasa Mjerumani huyo anapokea Pauni 135,000 (zaidi ya Sh mil. 430).

Wakati Rudiger akiweka sharti hilo, matajiri wa soka la Ufaransa, PSG, wanasikilizia kuona kama Chelsea watashindwa ili wao wajitose kumchukua.

Itakumbukwa kuwa mchezaji huyo alikuwa sehemu ya wachezaji waliotarajiwa kuondoka Stamford Bridge majira ya kiangazi, wakati huo akihusishwa zaidi na AC Milan.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles