22.3 C
Dar es Salaam
Wednesday, May 22, 2024

Contact us: [email protected]

Rais Samia kufuangua Jukwaa la Kodi na Uwekezaji

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

RAIS Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kufungua jukwaa la kodi na uwekezaji mwaka huu, lililoandaliwa na Wizara ya Fedha kwa lengo kusaidia kuandaa bajeti ya mwaka 2024/2025.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Elijah Mwandumbya.

Akizungumza jijini Arusha Februari 23, 2024 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Elijah Mwandumbya amesema jukwaa hilo ni utaratibu wa kawaida ambao unawahusisha wananchi na wadau wengi kutoa maoni yao.

Amesema jukwaa hilo litafanyika jijjni Dar es salaam na kushirikisha wadau 1000, wakiwemo wafanyabiashara,mabalozi, wadau sekta binafsi wa ndani na nje ya nchi.

“Mpaka sasa tumeshapita katika kanda mbalimbali nchini, kwa ajili ya kukusanya maoni ya wadau na wananchi na Februari 27 na 28 itakua ni hitimisho,” amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles