24.2 C
Dar es Salaam
Friday, October 18, 2024

Contact us: [email protected]

Kitwanga achangisha  milioni 28/- za sekondari

charles-kitwangaNa PETER FABIAN

MBUNGE wa   Misungwi, Charles Kitwanga (CCM) maarufu kama Mawematatu, amechangisha   Sh milioni 28 na mifuko 226 ya saruji  katika ujenzi wa shule ya sekondari ya kKata ya Gulumungu.

Katika harambee hiyo iliyofanyika katika Kijiji cha Nyamahinza,  Leticia Luboja (75) alijitokeza kumunga mkono kwa kuchangia mifuko mitano ya saruji.

Kitwanga alimuomba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Misungwi kuwakamata na kuwafikisha mahakamani haraka mwenyeviti wa Kijiji cha Gulumungu,   na wenyeviti wa vitongoji saba akidai wanakwamisha shughuli za maendeleo ikiwamo ujenzi wa sekondari hiyo.

Alisema anatambua Serikali haina fedha za kutosha kukamilisha kila kitu hivyo aliwaomba wananchi kujitokeza kuchangia miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na elimu.

“Sote tunafahamu changamoto za sekta ya elimu watoto kusomea katika mazingira yasiyo rafiki nitaendelea kuzungumza na marafiki zangu.

“Fedha hazitoshi, lakini kwa nguvu zetu zitatosha sasa nawaomba wale wenye nafasi na uwezo wa kuchangia mfanye hivyo na ukiitwa kuchimba msingi usiache kufanya hivyo,” alisema Kitwanga.

Kitwanga   alisema yeye na marafiki zake waliomuunga mkono katika ujenzi huo wamechangia   Sh milioni 11.7 na kati ya hizo Sh milioni 5.7 ni fedha tasilimu na ahadi zikiwa ni Sh milioni sita.

Alisema walioahidi ni kampuni mbalimbali wakiwamo rafiki zake na kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi imetoa mifuko 68 ya saruji ambayo itasaidia kukamilisha ujenzi huo.

Wananchi wa kata hiyo kwa pamoja walichangia Sh milioni 6,794,000  na kupitia Kamati ya Maendeleo ya Kata (WDC) Sh milioni 3.7.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Misungwi, Anthony Bahebe alisema kazi ya kujenga shule haiishi kwa siku moja.

Alisema  bila wananchi kusimama na kushikamana hakuna mtu wa   kuwasaidia bali  umoja wao utasaidia kukamilisha ujenzi huo.

Mkurugenzi wa Wilaya  ya Misungwi, Eliud Mwaiteleke alimshukuru Kitwanga kwa jitihada zake katika  kuleta maendeleo jimboni humo.

Vilevile aliwashukuru  wananchi kwa kujitolea na kuiunga mkono halmashauri  ili kufikia maendeleo katika nyanja zote.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
590,000SubscribersSubscribe

Latest Articles