24.1 C
Dar es Salaam
Sunday, May 19, 2024

Contact us: [email protected]

ECKERNFORDE, TANGA HOTELI WADAIWA SUGU WA KODI

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imekifungia Chuo Kikuu cha Eckernforde na taasisi zake kutokana na kuwa wadeni sugu wa kodi ya mapato kwa wafanyakazi (PAYE), kodi ya ongezeko la thamani (VAT) na kuendeleza ufundi stadi (SDL) tangu mwaka 2012 hadi mwaka 2016.

Meneja wa Mapato wa TRA, jijini humo Masawa Masatu amesema hayo leo baada ya kufungwa kwa chuo hicho ambapo pia mamlaka hiyo imeifungia Hoteli ya Tanga huku Meneja huyo akisisitiza kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu hadi wadaiwa wote sugu watakapolipa madeni yao.

“TRA imechukua hatua ya kufungia majengo yote matano yanayomilikiwa na taasisi hiyo ya elimu baada ya kubainika kuwa ni wadeni sugu na wamekuwa wakikaidi ulipaji kodi kwa miaka mingi,” amesema Masatu.

Hata hivyo, Meneja huyo alipotakiwa kutaja kiasi cha fedha inachodaiwa taasisi hiyo amesema taratibu haziruhusu kutokana na sheria ya takwimu kumbana.

Naye Mkuu wa chuo hicho, Profesa Kiango amesema hali hiyo imesababishwa na chuo kukosa wanafunzi kwa ambapo mwaka huu wa masomo kimepokea wanafunzi wachache huku wafanyakazi wa Tanga Hoteli wakilalamika kutolipwa mishahara tangu Julai, mwaka huu.

 

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles