LOS ANGELES, Marekani
STAA wa muziki nchini Marekani, Beyonce, amepata shavu la kuingiza wimbo katika filamu ya baba yake Serena Willliams, mzee Richard Williams.
Filamu hiyo iitwayo King Richard, inazungumzia maisha yam zee huyo na namna alivyoanza harakati za kuwafikisha kwenye mafanikio ya tenesi mabinti zake wawili; Serena na Venus.
Mwongozaji wa mzigo huo ni Reinaldo Marcus Green, huku mmoja ya waigizaji akiwa ni mkali wa vichekesho ambaye pia ni mwanamuziki, Will Smith.
Filamu hiyo ilitarajiwa kuingia sokoni Novemba 25, mwaka jana, lakini ilishindikana kutokanana ‘fujo’ za janga la Corona, hivyo kwa Marekani itaanza kuonekana Novemba 19, mwaka huu.