24.3 C
Dar es Salaam
Monday, September 16, 2024

Contact us: [email protected]

Bashe: Msiuze mashamba, tunzeni ardhi

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe (Mb) amemuelekeza Afisa Kilimo wa Kata ya Mwamkulu kuhakikisha anasimamia na kuhamasisha wakulima kujisajili kwa wingi katika mfumo wa ruzuku ya mbolea.

Waziri Bashe ameanza ziara yake ya kikazi Julai 19, 2024 katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, Mkoa wa Katavi na kuweka jiwe la msingi la Ujenzi katika Skimu ya Umwagiliaji ya Mwamkulu yenye ukubwa wa hekta 3,000 ambazo zitanufaisha wakulima takribani 20,000.

“Serikali imewekeza fedha nyingi, ni lazima kuwe na uwajibikaji wa kuhakikisha wakulima wananufaika. Kwa mfano, idadi ya wakulima waliojisajili kupata mbolea za ruzuku, kiasi cha uzalishaji na aina ya mazao ili ijulikane katika kufikisha huduma vijijini,” amesisitiza Waziri Bashe.

Pia Waziri Bashe amewaomba Wakulima wa Mpanda na Mkoa mzima wa Katavi kutouza ardhi. “Mradi huu ni wa kwenu. Msiuze mashamba. Tunzeni ardhi yenu isaidie vizazi vijavyo. Serikali imegharamia karibia Sh milioni 10 kwa kila hekta inatumika ili kuwasaidia shughuli zenu za uzalishaji na pia maeneo ya mifugo kupata maji,” amesema Bashe.

Aidha, ameelekeza Idara ya Maendeleo ya Mazao kuhakikisha kuwa ngazi za Mikoa na Halmashauri za Wilaya kufuatilia utendaji wa Maafisa Ugani kwa kutumia mfumo Maalum ambao umewekwa kwenye vishikwambi vinavyosambazwa na Wizara ya Kilimo kwa Maafisa Ugani. Pia amemuelekeza Mkurugenzi wa Idara ya Zana za Kilimo katika Wizara ya Kilimo kuhakikisha kuwa baada ya uzinduzi wa usambazaji wa trekta na “power tiller” mwezi Agosti 2024 zisambazwe kwa Wakuu wa Wilaya ikiwemo Mpanda ili kusaidia shughuli za kilimo kwa wakulima.

Waziri Bashe amelakiwa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuf kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi. Akitoa salamu za Mkoa, Jamila alieleza kuwa “Wilaya yetu ya Mpanda ni miongoni mwa maeneo yanayoongoza akiwa Kilimo cha mpunga. Tunatoa shukrani kwako na Wizara kwa ujumla kwa kuleta miradi ya ujenzi wa skimu za umwagiliaji kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa wakulima wetu ambayo ni skimu ya Mwamkulu kwa gharama ya Sh Bilioni 31.6 na skimu ya Usese kwa ajili ya ukarabati kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.2,” amesema Jamila Yusuf.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles