25.8 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Tuzo ya Amani yaja nchini

TUZO aMANNA ESTHER MNYIKA

SHIRIKA Linalohusika na Sekta Mtambuka (BBIO) limetambulisha tuzo mpya iitwayo ‘Amani Awards’, inayolenga kufikisha ujumbe wenye dhamira inayobeba kazi mbalimbali za kimuziki, filamu na habari kwa ujumla.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Shirika hilo, Amani Mgullo, alisema lengo la kuanzisha tuzo hizo ni kuchangia dhima ya maisha bora na dunia bora kwa kila mwanadamu.

Alisema hiyo ni kuchochea umahiri katika kutoa, kueneza na kufikisha ujumbe wa maendeleo endelevu kupitia tasnia za muziki, filamu na habari.

“Tafiti zimethibitisha kuwa tasnia za muziki, filamu na vyombo vya habari vina uwezo mkubwa wa ushawishi na kufikia watu wote, matajiri kwa masikini, wake kwa waume, viongozi kwa waongozaji na zinavuka mipaka ya kimataifa,” alifafanua Mgullo.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles