27.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

NI UHURU KENYATTA KENYA

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (IEBC), Wafula Chebukati amemtangaza Rais Uhuru Kenyatta kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais.

Chebukati amemtangaza Kenyatta chama Jubilee kwa kupata kura 8,203,290 sawa na asilimia 54.27 ya kura zote zilizopigwa huku mpinzani wake, Raila Odinga aliyekuwa anawakilisha Muungano wa vyama vya upinzani (NASA), akipata kura 6,762,224 sawa na asilimia 44.74 ya kura zote zilizopigwa.

Aidha, watu waliojitokeza kupiga kura walikuwa 15,073,662 sawa na asilimia 78.91 kati ya milioni 19 waliojiandikisha kupiga kura huku kura zilizoharibika zikiwa 399, 935.

Licha ya mchuano mkali ambao ulionyesha tangu awali Kenyatta akiongoza lakini Raila na wafuasi wake waliamini ameshinda uchaguzi huo huku akitaka tume imtangaze kuwa mshindi wa urais.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles