STAA wa PSG, Lionel Messi, amekiri kuwa kitendo cha kufunga bao la kwanza akiwa na uzi wa timu hiyo kimemwondoshea msongo wa mawazo.
Messi aliyeifungia PSG jana katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Manchester City, amesema aliteseka kuona anachelewa kufungua akaunti ya mabao jijini Paris.
“Ni kweli kwamba nilikuwa najisikia vibaya kutoanza kufunga,” amesema Messi akihojiwa na kituo cha televisheni cha Canal Plus.
Kwa upande wake, kocha wa PSG, Mauricio Pochettino, amesema huwa hashangilii mabao lakini bao la Messi lilimfanya aachane na utamaduni wake huo.