LOS ANGELES, Marekani
MWANAMITINDO mwenye jina kubwa nchini Marekani, Gigi Hadid, ametemana na mpenzi wake, Zayn Malik, kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na jarida la People.
Kile kilichoelezwa na chanzo cha habari hicho ni kwamba wapenzi hao wa muda mrefu wameachana baada ya mshikaji, Malik, kugombana na mama mkwe, Yolanda.
Alipoulizwa juu ya bifu la Malik na ‘bi mkubwa’, Gigi amesema kwa sasa hatazungumzia hilo na badala yake ameelekeza akili yake kwenye malezi ya binti yake mwenye umri wa miezi 13, Khai.
Aidha, mtu wa karibu wa Gigi aliyehojiwa na jarida jingine, PageSix, amesema: “Kwa sasa hawako pamoja. Lakini wote ni wazazi wazuri (kwa binti yao).”