LOS ANGELES, Marekani
MTOTO wa kike wa Floyd Mayweather, Yaya, anashutumiwa kwa kumchoma kwa kitu chenye ncha kali mwanamke anayefahamika kwa jina la Lapattra Jacobs.
Kwa mujibu wa kile kilichoelezwa, Yaya mwenye umri wa miaka 21, huenda akahukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani endapo atakutwa na hatua katika kesi hiyo itakayoanza kusikilizwa Februari, mwakani.
Kama ilivyo Yaya, Lapattra amezaa na rapa YoungBoy na tukio la wao kukwaruzana lilitokea Aprili, mwaka jana, siku ambayo mshikaji naye alikuwepo.
Haya ni majanga kwa wapenzi hao, Yaya na YoungBoy, kwani jamaa naye anasubiri kesi yake ya kuuza dawa za kulevya na kumiliki silaha iliyoibiwa.