CATALUNYA, Hispania
UKIACHA Hakim Ziyech, pia Barcelona wamepanga kuibomoa Chelsea kwa kumchukua staa mwingine wa timu hiyo ifikapo Januari, mwakani.
Kwa mujibu wa taarifa, nyota aliyeingia kwenye rada za vigogo hao wa La Liga ni straika wa Kijerumani, Timo Werner.
Barca wamewageukia wawili hao baada ya kuona haitakuwa rahisi kwa Manchester City kumwachia mshambuliaji raia wa England, Raheem Sterling.