MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ambwene Yessayah (AY), amesema amekaa muda mrefu bila ya kuoa kutokana na kukosa mwanamke mwenye sifa atakazo.
AY amedai kwamba, amekutana na wanawake wengi lakini bado hajapata yule mwenye sifa ambazo anaweza kuridhika naye na kuweza kumuoa.
“Kuna wanawake wengi ambao wanaonekana kama wanafaa kuolewa, lakini kwa upande wangu bado sijakutana na yule ambaye ananifaa kumuoa, hadi sasa ninaishi bila mwanamke tangu miaka miwili iliyopita baada ya kuachana.
“Wakati niko naye nilijiambia kwamba huyu ni mwanamke sahihi wa kumuoa, lakini sio kweli na mara baada ya muda tulishindwana na kila mtu anaishi kivyake, nitakuja kuoa mwanamke ambaye anajielewa na kujipenda,” alisema AY.