27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

AY aeleza sifa za mwanamke wa kuoa

ayNA MWANDISHI WETU

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ambwene Yessayah (AY), amesema amekaa muda mrefu bila ya kuoa kutokana na kukosa mwanamke mwenye sifa atakazo.

AY amedai kwamba, amekutana na wanawake wengi lakini bado hajapata yule mwenye sifa ambazo anaweza kuridhika naye na kuweza kumuoa.

“Kuna wanawake wengi ambao wanaonekana kama wanafaa kuolewa, lakini kwa upande wangu bado sijakutana na yule ambaye ananifaa kumuoa, hadi sasa ninaishi bila mwanamke tangu miaka miwili iliyopita baada ya kuachana.

“Wakati niko naye nilijiambia kwamba huyu ni mwanamke sahihi wa kumuoa, lakini sio kweli na mara baada ya muda tulishindwana na kila mtu anaishi kivyake, nitakuja kuoa mwanamke ambaye anajielewa na kujipenda,” alisema AY.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles