25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Yanga yaendelea kuwaumiza

Na Winfrida Mtoi, Mtanzania Digital

TIMU ya Yanga imeendelea kujichukulia pointi tatu katika michezo yake ya Ligi Kuu Tanzania Bara, leo Novemba 2, 2021 ikiichapa Ruvu Shooting mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

Ruvu ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya tisa kupitia Shaban Msala, kabla ya Feisal Salum “Fei Toto” kuisawazishia Yanga dakika ya 33.

Bao la pili limefungwa kwa mkwaju wa penalti na Djuma Shaaban dakika ya 48 baada ya beki wa Ruvu Shooting Ally Mtoni ‘Sonso’ kuunawa mpira, kisha Mukoko Tonombe dakika ya 75, hivyo kuwafanya wananchi kuendelea kukaa kilele kwa kufikisha ponti 15 baada ya kushinda michezo mitano mfululizo.

Beki wa Ruvu Santos Mazengo alioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumfanyia madhabi mchezaji wa Yanga, hivyo kuwafanya maafande hao wanaonolewa na Charles Mkwasa kucheza  wakiwa pungufu.  

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles