23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

WENYE ULEMAVU WALILIA  MIUNDOMBINU RAFIKI 

Na CLARA MATIMO-  MWANZA


 

walemavuWAKAZI wa Kata ya Kayenze Wilaya ya Ilemela   wameiomba Serikali kufanya maboresho katika sekta ya afya ili huduma zinazotolewa kuanzia zahanati hadi hospitali za rufaa za mikoa na taifa zizingatie mahitaji ya watu wenye ulemavu.

Ombi hilo lilitolewa jijini   hivi karibuni  kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama  cha Watu Wenye Ulemavu Tanzania (CHAWATA) Wilaya ya Ilemela ambao ulilenga kuwaelimisha jamii kuhusu haki za  watu wenye ulemavu.

Walisema  watu wenye ulemavu hupata changamoto mbalimbali  wanapokwenda kupata huduma za afya kutokana na maeneo mengi yanayohudumia jamii mbalimbali kutozingatia mahitaji ya  makundi maalum.

“Ukienda kwenye hospitali za serikali hakuna hata wataalamu wa afya ambao wanaelewa lugha za  alama wakati inatakiwa wawepo kwa sababu nchi yetu ilikwisha kusaini mkataba wa kimataifa wa watu wenye ulemavu.

“Hivyo ni lazima kila jambo la maendeleo linalofanywa  lizingatie mahitaji maalum yanayowahusu watu hao.

“Pia nchi yetu ina sera ya  watu wenye ulemavu  ya mwaka 2009 na sheria yake ya mwaka 2010 lengo la yote haya ni kuhakikisha haki za watu wenye ulemavu zinalindwa.

“Sasa kama tutawanyanyapaa kuanzia kwenye huduma za umma na jamii ambazo ni muhimu kwa maisha ya kila siku  nani atawasaidia?” alihoji  Belita Misalaba.

Mwenyekiti wa Chawata Kata ya Kayenze, Ally Salum,  aliwataka   madereva  kuwa makini wanapoendesha vyombo  vya  moto   kuepuka kuongeza idadi ya watu wenye ulemavu katika jamii.

Mwezeshaji wa  mkutano huo kutoka Chawata Ilemela, Adam Ndokeji, alisema  ni wajibu wa jamii kuwalinda watu wenye ulemavu kwa kuhakikisha miundombinu ya barabara, vyoo, shule na ofisi za serikali zinajengwa kwa kuzingatia mahitaji ya watu hao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles