30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Usiombe kukutwa mechi ya watani

kamishina sirroNa Asifiwe George, Dar es Salaam

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, limejipanga kuhakikisha  mchezo wa Simba na Yanga utakaochezwa Februari 20 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa unachezwa  katika hali ya amani na usalama.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro, alisema mashabiki wa timu hizo hawataruhusiwa kuingia uwanjani na chupa za maji, silaha ya aina yoyote na hawatoruhusiwa kupaki magari ndani ya uwanja isipokuwa maeneo maalumu tu.

Kamanda Sirro alisema barabara zote zinazoingia katika uwanja huo zitafungwa ili kupisha msongamano wa magari, pia kutakuwa na ukaguzi mkali  katika milango yote mikubwa  ili kuhakikisha wanaoingia  uwanjani hapo hawana vitu vyenye uwezekano wa kuleta madhara kwa watazamaji.

“Ninawashauri wananchi kukata tiketi zao mapema kwenye vituo  vilivyoainishwa na vyombo husika ili kuepuka usumbufu  usiokuwa wa lazima na wale watakaolazimika kukata tiketi uwanjani hapo ninawashauri  kufuata  utaratibu uliopangwa.

“Kutakuwa na kamera za CCTV zitakazofungwa kuzunguka uwanja wote ili kusaidia kuimarisha ulinzi  katika mechi hiyo, hivyo matukio yote muhimu yatarekodiwa,” alisema Kamanda Sirro.

Kamanda Sirro alisema kutakuwa na doria za mbwa wa polisi na farasi waliopata mafunzo ya kisasa ambao watazunguka nje ya uwanja kuimarisha  ulinzi ili kuhakikisha mechi hiyo inamalizika kwa amani na utulivu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles