23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

United yatabiriwa majanga

MANCHESTER, England

MANCHESTER United itamaliza msimu huu ikiwa nafasi ya saba kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England endapo itaendelea kumng’ang’ania kocha aliyeko sasa, Ole Gunnar Solskjaer.

Aliyeyasema hayo ni Darren Bent, mpachikaji mabao wa zamani aliyewahi kutamba England akiwa na Tottenham, Sunderland, na Aston Villa kwa kuzitaja kwa uchache.

Mashetani Wekundu wako kwenye hali mbaya msimu huu kwani wameambulia pointi moja tu katika mechi za Ligi Kuu walizocheza hivi karibuni, ikiwamo ile ya kutandikwa mabao 5-0 na Liverpool wikiendi iliyopita.

Akihojiwa na kituo cha televisheni cha talkSPORT, Bent amesema: “Watamaliza wakiwa nafasi ya saba. Kama wataendelea kuwa na Solskjaer msimu mzima, kiukweli watakuwa nafasi ya saba.”

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles