26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Ugonjwa hatari kwa watoto wagundulika

mtoto*Matibabu yake hugharimu Sh milioni 4 kwa wiki

Na CLARA MATIMO-MWANZA

CHUO Kikuu cha Sayansi ya Afya na Tiba cha Bugando (CUHAS), kimegundua kuwapo  maambukizi ya bakteria mpya aina ya enterobacter bugandesis ambao huwaathiri watoto njiti na walio na umri chini ya mwezi mmoja.

CUHAS wanasema matibabu ya maambukizi hayo hugharimu Sh milioni 4.5.

Akizungumza  na waandishi wa habari jana, Naibu Makamu Mkuu, Taaluma na Utafiti wa CUHAS, Profesa Stephen Mshana,  alisema bakteria hao husababisha maambukizi ya ugonjwa (Neonatal Sepsis) ambao dalili zake ni kupata homa kali, degedege, kupumua kwa taabu na kushindwa kunyonya.

Alisema katika utafiti wao wamebaini asilimia tano ya watoto walio na  umri chini ya mwezi mmoja ambao hutibiwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando (BMC) wameathiriwa na enterobacter bugandesis.

Alisema bakteria huyo husababishwa na matumizi yasiyo sahihi ya dawa kwa muda sahihi na matumizi ya dawa yasiyoidhinishwa na daktari.

Profesa Mshana alisema bakteria hao ni sugu lakini hutibika ila matibabu yake ni ghali ambapo chupa moja ya dawa huuzwa kwa Sh 300,000 na mgonjwa huhitaji chupa 10 hadi 15 kwa matibabu ya siku saba.

“Dawa zinazotibu ugonjwa unaosababishwa na bakteria enterobacter bugandesis ni ghali na Watanzania wengi hawawezi kumudu. Chupa moja ya dawa inafika hadi Sh 300,000, mtoto akipatwa na tatizo hili kwa wiki moja anaweza kuhitaji chupa 10 hadi 15,” alisema.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC), Lucy Mogele, alisema katika kipindi cha mwaka 2015 walipokea watoto 240 walio na umri chini ya miezi miwili ambapo kati yao watoto 12 waligundulika kuwa na bakteria hao, mwaka huu tangu Januari hadi  Oktoba wamepokea watoto 180 na watoto tisa wamebainika kuwa na maambukizi.

Akizungumzia mafanikio ya chuo hicho, Makamu  Mkuu wa CUHAS, Profesa Paschalis Rugarabamu, alisema tangu kuanzishwa kwake mwaka 2003 kimetoa  madaktari bingwa 111  kati yao wamo wa magonjwa ya akina mama, afya ya watoto, utabibu na upasuaji ingawa idadi hiyo haikidhi mahitaji ya taifa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles