KINGSTON, Jamaica
LEJENDARI wa muziki wa reggae nchini Jamaica, Robbie Shakespeare, ameiaga dunia akiwa na umri wa miaka 68.
Shakespeare aliyekuwa mkali wa gitaa, ambapo alishinda tuzo mbili za Grammy, alifariki alipokuwa akiendelea na matibabu ya figo mjini Florida, Marekani.
Waziri wa Utamaduni wa Jamaica, Olivia Grange, amemtaja Shakespeare kuwa mmoja wa nembo za muziki zilizowahi kutokea katika Kisiwa hicho.
Katika miaka yake takribani 50 kwenye muziki, Shakespeare alishirikiana na mastaa wengi wa muziki, wakiwamo Madonna na Peter Tosh.