28.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Sitta: Nitadumisha Muungano

samwel-sittaNa Joseph Manyonyi, Bunda

WAZIRI wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Samuel Sitta, amesema ataendelea kudumisha na kulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ikiwa atapewa ridhaa ya kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Sitta alisema hayo juzi, wakati akiwashukuru wanachama wa CCM wa Wilaya ya Bunda waliofika kumdhamini ili ateuliwe kuwa mgombea urais, shughuli iliyofanyika katika kiwanja cha Ofisi ya CCM Wilaya ya Bunda, mkoani Mara.
Mgombea huyo alisema ataulinda Muungano wa Tanzania na kuendeleza mema yote ya muungano huo kama ulivyoasisiwa na waasisi ambao ni hayati Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Karume, kwa manufaa ya pande zote mbili za nchi yetu.
Kuhusu katiba, alisema atasimamia uboreshaji wa katiba ya wananchi ambayo tayari imekwisha pitishwa na Bunge Maalumu la Katiba, ambalo yeye alikuwa mwenyekiti ili kuwapa haki wananchi wanaoishi Tanzania bara na visiwani.
Alitoa mfano kuwa, Katiba mbaya husababisha umwagaji wa damu na wananchi kuwa wakimbizi nchini mwao, kama vile Burundi ambako hivi sasa wananchi wanaikimbia nchi hiyo, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles