LOS ANGELES, Marekani
IKIWA ni miaka minne tangu aliposajiliwa, rapa Big Sean ametangaza kuachana na lebo ya G.O.O.D. Music inayomilikiwa na staa wa muziki, Kanye West.
Akiwaambia mashabiki wake kupitia ukurasa wa Twitter jana, Sean amesema uamuzi huo haujatokana na ugomvi, bali ni katika kujitanua zaidi kimuziki.
Akiwa na G.O.O.D. Music, alifanya vizuri sokoni, ikiwamo albamu yake ya ‘Detroit 2’, na sasa ataendelea kufanya kazi na lebo nyingine kubwa, Def Jam Recordings.
Tayari ameshaachia ‘EP’inayokwenda kwa jina la ‘What You Expect’ikiwa na ngoma sita, ambayo prodyuza wake ni Hit-Boy ambaye ndiye aliyesimamia albamu yake kali ya ‘Detroit 2’.