LOS ANGELES, Marekani
MWIGIZAJI ambaye pia ni rapa, Ice Cube, amekubali kuzikosa Dola milioni tisa (zaidi ya Sh bil. 20 za Tanzania) baada ya kukataa kucheza filamu aliyolazimishwa kupata chanjo ya Corona.
Cube mwenye umri wa miaka 52, alifuatwa na maprodyuza wa filamu hiyo ya vichekesho lakini walishindwana naye walipomwambia atachanjwa kabla ya kuingia ‘lokesheni’.
Filamu hiyo iitwayo ‘Oh Hell No’inatarajiwa kuanza kurekodiwa Hawaii mwanzoni mwa mwaka ujao, huku lokesheni ya kwanza ikiwa Hawaii, eneo ambalo asilimia 90 ya wakazi wake wenye umri kuanzia miaka 12 wameshachanjwa.