23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

RIHANNA AONYESHA JEURI YA FEDHA

California, marekani

MSANII wa muziki wa Pop nchini Marekani, Rihanna Fenty, ameonesha jeuri ya fedha kwa kutumia dola milioni 6.8, zaidi ya bilioni 13 kununua nyumba.

Nyumba hiyo amenunua katika eneo la West Hollywood, mjini California karibu na ilipokuwa nyumba ya mwanamitindo Kendall Jenner. Nyumba hiyo ina jumla ya vyumba sita vya kulala, eneo la nyumba hiyo lina ukubwa wa mita 18,000.

Rihanna alitumia ukurasa wake wa Instagram kuionesha nyumba hiyo huku akidai anafurahia kuamini makazi mapya.

“Furaha yangu ni kuona kwamba nina sehemu ambayo ninaweza kuziweka gari zaidi ya nane, sehemu ya mazoezi pamoja na mambo mengine mengi, ni furaha kuwa na sehemu kama hii ya ndoto zangu,” aliandika Rihanna.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles