25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Rangnick kumbakiza Cavani

MANCHESTER, England

MKUU wa benchi la ufundi la Manchester United, Ralf Rangnick, amesema anataka kuona straika mkongwe, Edinson Cavani, akimaliza msimu huu akiwa klabuni hapo.

Cavani (34), amekuwa akihusihwa na mpango wa kuondoka Old Trafford kupitia usajili wa dirisha dogo la Januari, mwakani.

Licha ya kuanza vizuri katika siku za mwanzoni mwa kibarua chake Old Trafford, Cavani alijikuta akipoteza nafasi ya kucheza, hasa baada ya usajili wa Cristiano Ronaldo.

Barcelona imekuwa mstari wa mbele kuifukuzia saini ya Cavani lakini Rangnick haoneshi kuwa anataka kumwachia nyota huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles