KOCHA wa PSG, Mauricio Pochettino, amesema usajili wa Lionel Messi klabuni hapo ulimwacha mdomo wazi kwa kuwa hakuutarajia.
“Sikudhani kama ingewezekana (Messi kutua PSG)… Nimekuwa nikivutiwa naye kwa muda mrefu, tangu nilipokuwa nakutana naye kama mpinzani. Kwa hiyo, ni jambo zuri sana kuwa naye mazoezini. Nafikiri tukiwa pamoja tutafikia ndoto ya klabu.”
Messi (34), aliondoka Barca wakati wa usajili wa kiangazi, mwaka huu, na hiyo ilitokana na ukata unaoiyumbisha klabu kongwe hiyo katika historia ya Ligi Kuu ya Hispania (La Liga).
Ukimlinganisha na Pochettino, si tu wote ni Waargentina, bali pia wawili hao ni mashabiki wakubwa wa klabu ya nchini kwao, Newell’s Old Boys, huku wakiwa ni wazawa wa Mji mmoja; Rosario.