24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

PNC awalalamikia wasanii wenzake

Na GLORY MLAY

MSANII wa Bongo Fleva, Pancras Charlz, maarufu PNC, amsema wasanii wanaotoa nyimbo kila mara wanasababisha soko la muziki hapa nchini kupoteza muelekeo.

Akizungumza na MTANZANIA jana, PNC alisema, msanii ambaye anajitambua na kujua nini anafanya anatakiwa kuachia wimbo mmoja kwa mwaka au miezi sita ili kuupa nafasi ya kusikilizwa na mashabiki.

“Soko linakufa maana wasanii kwa sasa kama wanashindana, kila mwezi anatoa ngoma, msanii unatakiwa unakaa mwaka mmoja ndio unaachia nyingine ili wimbo huo uishi kwa mashabiki, lakini kutoa kila mara kuna sababisha kupoteza maana ya bongo fleva.

“Wakati mwingine nyimbo hizo hazina ubora wowote ili mradi na yeye anaonekane kwenye Tv au watu wamsikie mtaana lakini hajui kwamba muziki unakufa, tungo zao hazina ubora wanarudia maneno yale yale na nirahisi kupotea masikio mwa watu maana hatojua asikile upi aache upi,” alisema msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles