23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Cardi B azalilika jukwaani

NASHVILLE, MAREKANI

RAPA Cardi B, mwishoni mwa wiki iliopita alizalilika baada ya nguo aliyovaa kuchanika jukwaani wakati wa tamasha la 2019 Bonnaroo Arts And Music.

Msanii huyo alipanda jukwaani ikiwa ni mara yake ya pili baada ya kusitisha kufanya muziki kwa wiki kadhaa kutokana na hali yake kutokaa vizuri tangu afanyiwe upasuaji wa miguu, matit na makalio.

Mbali na kufanya shoo ya aina yake, lakini msanii huyo alijikuta na aibu baada ya nguo yake kuchanika kwenye makalio. Msanii huyo aliamua kuivua na kuendelea na burudani kama kawaida.

Muda mchache baadae picha za msanii huyo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii, lakini mwenyewe hakuonesha kama lilikuwa tatizo kubwa, alionekana kufurahia kitendo cha mashabiki kulizungumzia suala hilo huku akidai mwili wake umekuwa mkubwa na ndio maana ilichanika.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles