Sharifa Mmasi,Mtanzania DigitalÂ
MCHEZAJI nyota wa gofu hapa nchini, Seif Mcharo amesema yupo katika maandalizi ya nguvu tayari kwa kukabiliana na mashindano yoyote mbele yake ili kufanya vizuri.
Akizungumza na Mtanzania Digital jana, Mcharo amesema kuwa ili mchezaji afanye vema kwenye michuano anapaswa kujiandaa muda mrefu ndiyo sababu ameamua kutumia muda mwingi uwanjani kujifua.
” Kwa sasa sina ratiba ya mashindano yoyote yale lakini binafsi bado naendelea na mazoezi ya kila siku lengo ni kujifua na kujiweka tayari na lolote.
” Mchezo wa gofu unahitaji mchezaji awe fiti muda wote ndio maana naituma mazoezini ili yakitokea mashindano ili niibuke kidedea,” amesema Mcharo.