Sharifa Mmasi, Mtanzania Digital
UONGOZI wa Chama cha Mchezo wa Judo Tanzania ( JATA), umewataka wachezaji wa klabu zote nchini, kuendelea kufanya mazoezi yenye viwango vya hali ya juu lengo ni kujiweka fiti tayari kwa mashindano ya klabu.
Mashindano hayo yanayohusisha klabu mbalimbali za Tanzania, yamepangwa kufanyika Oktoba 10-11 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mtanzania Digital, Katibu Mkuu wa JATA, Innocenta Malya amesema mashindano hayo yataonyeshwa mubashara kupitia runinga ya Azam.
Aidha, amesema lengo la mashindano hayo ni kusaka wachezaji wenye viwango kwa ajili ya kuunda timu ya taifa ya Tanzania itakayoshiriki michuano ya Afrika Mashariki 2022 nchini Uganda.