24.1 C
Dar es Salaam
Sunday, May 19, 2024

Contact us: [email protected]

Ntibazonkiza, Mayele waing’arisha Yanga, Nabi aiweka Simba kiporo

Na Mwandishi Wetu, Mbeya

MABAO mawili ya Saido Ntibazonkiza na Fiston Mayele, yametosha kuipa Yanga alama tatu muhimu baada ya kuifunga Mbeya Kwanza mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Novemba 30,2021 kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Ntibazonkiza ndiye alianza kuwainua mashabiki wa Yanga  dakika ya  18 kwa mpira wa adhabu  baada ya Feisal Salum ‘’Fei Toto’kufanyiwa madhabi na mabeki wa Mbeya Kwanza, huku Mayele akifunga dakika ya 27 akipata pasi nzuri Fei Toto.

Saido Ntibazonkiza akishangilia baada ya kufunga bao

Ushindi huo umeifanya Yanga kuvunja rekodi ya Mbeya Kwanza ya kutopoteza mechi hata moja tangu imeanza ligi hiyo, huku Wanajangwani hao wakiendelea kujikita kileleni wakifikisha alama 19.

Kocha Mkuu wa Yanga, Nasredine Nabi, amesema baada ya   kutoka sare na Namungo katika mchezo uliopita alichukua jukumu la kurekebisha makosa.

 Mchezo ujao Yanga inakutana na Simba Desemba 11,2021 lakini kocha  huo amesema atauzungumzia baada ya mapumziko ya siku chache.

“Sasa hivi tunazungumzia ushindi wetu wa Mbeya Kwanza, najua mchezo ujao na Simba, nitauzungumzia baadae sio sasa,” amesema.

Kikosi cha Yanga kilichoanza leo

Kwa upande wa Kocha Mkuu wa Mbeya Kwanza, Hererimana Haruna, amesema wachezaji wake walikosa umakini, pia waamuzi hawakuwatendea haki.

Kikosi cha Mbeya Kwanza

Katika mchezo mwingine, Biashara United imelazimishwa sare ya bao 1-1 na Polisi Tanzania  kwenye Uwanja wa Karume, Mara.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles